Tarehe 21/11/2025 mwalimu mkuu amefanya kikao Cha wazazi wa darasa la sita na kueleza mikakati mbalimbali ya kuinua Taaluma na kukuza ufaulu kwa darasa la sita
Katika kikao hicho mwalimu mkuu ameongelea mambo mbalimbali kama ifuayavyo
1.Kuwajali wanafunzi kwa kuwanunulia vifaa vya kujifunzia na sare za shule
2.Kuwafaatilia watoto wao maendeleo ya shule kwa kutumia mfumo wa matokeo unaoitwa mwanzugi.com
3.Kuwa karibu baina ya mzazi na Walimu ili kumuendeleza mwanafunzi
Pia wazazi wamekubaliana kuwa wanafunzi wa Darasa la sita wasifunge shule na wasome kwa wiki tatu wakati wa likizo
Pia Kuwanunulia wanafunzi vifaa vifuatavyo
1.counter book query 3 saba
2.Daftari za msomi saba kwa ajili ya majaribio
3.Kuchangia kiasi cha Tsh. 5,000/= kwa ajili ya mitihani na motisha kwa walimu watakaokuwa wanafundisha wakati wa likizo
Pia mwalimu mkuu amewaomba wazazi kuisemea vizuri shule ya Msingi mwanzugi ili iweze kutangazika vyema
*Ufafanuzi wa Kalenda ya Masomo kwa Mwaka 2026 – Tanzania*
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na *Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia*, mwaka wa masomo 2026 kwa shule za awali, msingi na sekondari umegawanyika katika mihula miwili kama ifuatavyo:
*Muhula wa Kwanza (Muhula I):*
- *Unanza:* 13 Januari 2026
- *Likizo fupi:* 27 Machi – 07 Aprili 2026
- *Unafungwa rasmi:* 05 Juni 2026
- *Idadi ya siku za masomo:* 96
*Muhula wa Pili (Muhula II):*
- *Unanza:* 06 Julai 2026
- *Likizo fupi:* 04 – 13 Septemba 2026
- *Unafungwa rasmi:* 04 Desemba 2026
- *Idadi ya siku za masomo:* 98
*Jumla ya Siku za Masomo kwa Mwaka Mzima:*
- *194 siku*
*Maana yake:* Mwaka 2026 kutakuwa na vipindi viwili vya masomo vyenye likizo fupi katikati, na shule zinatarajiwa kufundisha kwa siku 194 jumla. Wazazi, walimu na wanafunzi wanashauriwa kufuata ratiba hii kwa ukamilifu ili kufanikisha malengo ya kitaaluma.
Wito wa mkutano mkuu wa Wazazi/Walezi
Posted on November 20, 2025, 10:07 amWalimu wakitimiza wajibu wao kwa kuwapima wanafunzi uwezo wa kusoma na kurekodi alama zao walizozipata
Posted on November 20, 2025, 8:47 amAngalia matokeo ya Mtihani wa Taifa wa darasa la saba 2025 Shule ya Msingi Mwanzugi.
Fungua File hilo hapo chini
Unakaribishwa kwa heshima kubwa kuhudhuria sherehe ya kuhitimu Darasa la Saba.
Tukio: Sherehe ya Kuaga Darasa la Saba
Tarehe: Jumamosi, 11 Oktoba 2025
Muda: Kuanzia saa 5:00 asubuhi
Mahali: Ukumbi wa St. Joseph
Ni furaha yetu kubwa kushiriki nawe siku hii ya pekee. Tafadhali fika kwa wakati.
Karibu Sana!